Kwa niaba ya uongozi wa Jumuiya ya Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDASA) kwa kushirikiana na Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala napenda kuwakaribisha kwenye  Kongamano la Muungano litakalofanyika ndani ya ukumbi wa Nkrumah siku ya Jumamosi tarehe 26 Aprili 2014. 
Kongamano hilo litaanza saa 7.30 mchana hadi saa 12 jioni ndani ya UKUMBI  WA NKRUMAH WA CHUO KIKUU CHA DARE ES SALAAM. Mada kuu ya Kongamano hilo ni, «Tujadili na Tutafakari Mustakabali wa Muungano wetu»

Kutakuwa na mada tatu za kujadiliwa na watoa mada kwenye mabano:

1)      Chanzo au Mchakato wa Kisiasa wa kuwa na Muungano ( Prof. Mohammed Bakari)
2)      Tathmini ya Miaka 50 ya Muungano (Dkt Alexander Makulilo)
3)      Mustakabali wa Muungano (Prof. Gaudence Mpangala)

Tunaomba kwa yeyote mwenye maoni basi asisite kututumia kwa barua pepe kwa anwani : kongamanoudasa@gmail.com.
  
Asanteni sana
 Bw. Faraja Kristomus
(Katibu – UDASA)
 0787 52 53 96 / 0717 086 135 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...