Mhe. Sophia M. Simba (Mb) na Familia yake,  anatoa shukrani zake za dhati kwa wote walioshirikiana naye katika kipindi kigumu cha kumuuguza mtoto wake mpendwa LEEFORD C. CENGE SIMBA (pichani), hadi alipoiaga dunia tarehe 06 Machi, 2014 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na kuzikwa tarehe 08 Machi, 2014 katika makaburi ya Kinondoni.

Kwa heshima kubwa tunatoa shukrani  za dhati  kwa Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mohamed Gharib Bilal Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Marais wastaafu ,Mhe. Benjamin William Mkapa  na  Mhe. Ali H. Mwinyi,  Mhe, Mizengo K. P. Pinda Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, IGP Ernest Mangu , Mhe.  Meck Sadick  Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Uongozi na Wafanya kazi wote wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto,Wahe. Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, majirani, ndugu, marafiki wa Masaki, Magomeni, Ilala Upanga,  na sehemu mbalimbali za  Dar es salaam na Tanzania kwa ujumla,  na wale wote wenye mapenzi mema kwa sala na dua zao katika kipindi hiki kigumu.

Shukrani za pekee ziwaendee Madaktari na wafanya kazi wote wa Hospitali ya Shri HinduMandal chini ya uongozi wa Daktari Kaushik akishirikiana na Madaktari mahiri, Dr Amar na Dr Mwanaada, na vilevile sista Mapunda kwa upendo na  huduma nzuri aliyoitoa.

Kwa vile si rahisi kumshukuru kila mmoja, tunaomba mkubali shukrani zetu za dhati kwa kushirikiana nasi katika mazishi ya kijana wetu.

Aidha tunaushukuru uongozi wa kanisa katoliki la Mashahidi wa Uganda  Magomeni na kanisa la Mtakatifu  Petro la Oysterbay kwa kuendesha Ibada ya mazishi.
Tunawakaribisha  kujumuika nasi katika Ibada ya Misa Takatifu ya kumuombea Marehemu, itakayofanyika katika kanisa Katoliki la Mashahidi wa Uganda  - Magomeni, Dar es salaam tarehe 27 Aprili, 2014 saa 02.30 asubuhi.
Tutahitimisha kwa chakula cha mchana, nyumbani kwa Mhe. Sophia M. Simba –Masaki Dar es salaam saa 6.00 mchana.  Tunawaomba mjumuike nasi.
 BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA,
JINA LA BWANA LIHIMIDIWE (JOB 1:21)


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...