Bendi Mahiri na Machachari Jijini Dar Skylight Band wametoa wimbo wao wa Tano ikiwa ni muendelezo wa kutoa nyimbo tofauti tofauti kupitia Studio yao ya kisasa ya Skylight Production.
Akiongea na Mtandao huu Meneja wa Band hiyo Aneth Kushaba AK47 amesema wimbo huo unaitwa “Pasua Twende” ambo umetungwa na Mkurugenzi Mkuu wa bendi hiyo Dk. Sebastian Ndege akishirikiana na wanamuziki wa Bendi hiyo.
Aneth akaongezea kwamba wimbo huo ni wa tano kutolewa katika mtiririko wa nyimbo zao zilizokwisha kutoka na imetengenezwa ndani ya studio yao ya Skylight Production chini ya Produzya Joobanjo.
Isikilize hapa chini na Ijumaa hii utapa fursa ya kusikiliza ikipigwa LIVE ndani ya kiota cha Thai Village Masaki jijini Dar.
Hapa Skylight Malaika Band mgefanya guitar la bass kusikika zaidi ya drums, sauti za waimbaji na organ, wimbo huu ungefanya vizuri zaidi na zaidi .
ReplyDeletelakini bado hamjachelewa mtakapotoa video/final edition ya huu wimbo guitar la bass liwe ndiyo linasikika kwa nguvu zaidi bila haja ya Dj au msikilizaji kutumia technolojia kunogesha.