Tanzania
imepandishwa hadhi katika Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na sasa inaweza
kupata mikopo mikubwa zaidi na yenye hadhi kubwa zaidi kuliko huko nyuma.
Mwakilishi Mkazi wa Benki hiyo katika Tanzania, Bi. Tonia Kandiero ametangaza
hayo, Julai 23, 2014.
Bi.
Kandiero amesema kuwa miaka yote tokea Tanzania kuwa mwanachama wa AfDB,
imekuwa inapata mikopo ya hadhi ya chini zaidi na midogo zaidi ya maendeleo kutokana
na uwezo na nguvu za uchumi wake.
Amesema
kuwa hadhi ya Tanzania ndani ya Benki hiyo imepanda kutokana na kukua kwa
uchumi wa Tanzania, kuongezeka kwa uwezo wa kukopesheka na uwezo wa kulipa na
kutimiza masharti yanayokwenda na mabadiliko hayo ya hadhi.
Bi.
Kandiero ametangaza mabadiliko hayo katika hadhi ya Tanzania ndani ya Benki
hiyo wakati alipozungumza katika sherehe kubwa ya kuweka jiwe la msingi kwenye
ujenzi wa Barabara ya Mangaka-Mtambaswala kwa kiwango cha lami na kufungua
Barabara ya Masasi-Mangaka ambayo imekamilika kwa kiwango cha lami.
Barabara
zote ziko katika mkoa wa Mtwara na mgeni
rasmi katika sherehe hiyo kubwa iliyofanyika mjini Mangaka, mji mkuu wa Wilaya
ya Nanyumbu, alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa.
Jakaya
Mrisho Kikwete, ambaye ameingia Mkoani Mtwara jana kwa ziara ya siku mbili. Ameingia Mtwara
akitokea Ruvuma ambako alifanya ziara ya siku sita.
Bi.
Kandiero amemwambia Rais Kikwete na mamia ya wananchi waliohudhuria sherehe
hiyo kuwa kabla ya kupandishwa hadhi, Tanzania ilikuwa na sifa za kukopa ndani
ya benki hiyo mikopo kutoka Mfuko wa Maendeleo wa Benki hiyo na siyo mikopo
mikubwa ya maendeleo.
Bi.
Kandiero amesema kuwa tokea Tanzania kujiunga na AfDB imepata kiasi cha mikopo
ya thamani ya zaidi ya dola za Marekani bilioni moja.
AfDB
ni moja ya wafadhili wa barabara hizo mbili ambazo sherehe zake za uzinduzi na
jiwe la msingi zimefanyika jana kwa kushirikiana na Serikali ya Japan kupitia
Shirika la Maendeleo la Japan (JICA) na Serikali ya Tanzania.
AfDB
na JICA zinashirikiana na Serikali ya Tanzania kugharimia ujenzi wa barabara
hizo chini ya Mradi wa kuendeleza Barabara nchini. Chini ya ushirikiano huo,
AfDB inatoa asilimia 64.79 kugarimia ujenzi wa barabara hizo, JICA inatoa asilimia 31.83 na Serikali ya
Tanzania inatoa asilimia 2.39.
Barabaraba
ya Mangaka-Mtambaswala, mpakani mwa Tanzania na Mozambique, ina urefu wa
kilomita 65.5, inajengwa na kampuni ya Jamhuri ya Watu wa China kwa gharama ya
shilingi bilioni 59.66 na ujenzi utakuchukua miezi 28.
Nayo
Barabara ya Mangaka-Masasi yenye urefu wa kilomita 55.1 ilikamilika mwanzoni
mwa mwaka huu baada ya kuwekewa jiwe la msingi la ujenzi wake na Rais Kikwete
Agosti 21, 2009. Barabara hiyo, ilijengwa na kampuni kutoka Japan kwa awamu
tatu na kwa gharama ya shilingi bilioni
54.8. Barabara hiyo ni sehemu ya
barabara ya Masasi-Mangaka-Tunduru.
Mapema
jana, Rais Kikwete amezindua mradi wa
maji wa Tarafa ya Nalasi mkoani Ruvuma mjini Nalasi, kilomita 12 kutoka mpakani
mwa Tanzania na Mozambique.
Mradi
huo ambao ni moja ya miradi inayofadhiliwa na Benki ya Dunia utawanufaisha watu
11,655 katika vijiji vitatu. Mradi huo una uwezo wa kutoa lita 200,000 za maji
ambayo yataweza kupatikana katika vituo
37 vya ugawaji maji. Ili kusambaza maji hayo kwa watu wengi zaidi, kiasi cha kilomita
14.5 ya mabomba yametandazwa katika vijiji hivyo.
Mradi
huo umejengwa na Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru kwa gharama ya sh milioni
445.
Imetolewa na;
Kurugenzi
ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es
Salaam.
24
Julai,2014
Hayo yote ni uongo. Hadhi imeongezeka jurikan na Tanzania kupata Gas asilia. Gas Asilia ndio Guarantee ya mikopo siku zinzokuja. Hiyo Banki imeipandishi Hahi Tanzani kwa maslhi yake.
ReplyDeleteMdau wa kwanza umesema ya ukweli,
ReplyDeleteNi wazi yakuwa tulipokuwa hatujapata Gesi asilia hatukuweza kukopesheka na sasa tumepata tunaweza kukopesheka!
Hata wewe ma mimi itakuwa ni vigumu kuamini kumkopesha Teja 'mla unga' ambaye hana dhamana, lakini pindi tukibaini yakuwa Teja amepata dhamana ama ameacha kula unga na kupata kazi ya kueleweka kimapato, vivyo hivyo na sisi tunaweza kumkopesha!
Heshima ya Tanzania umepanda saaana tu!
ReplyDeleteLicha ya changamoto chahce zilizopo ambazo hata duniani nchi zingine tena zilizoendelea zipo!
Mfano wa changamoto hizo ni mgawanyo wa Ukuzaji wa Kiuchumu (Less Inclusive Economic growth) tatizo ambalo hata Marekani,UK na Saudi Arabia yenye Uchumi wa mafuta miaka nenda miaka rudi wanalo tatizo hilo...Kama haiwezi kutokea Mfalme wa Saudi Arabia King Fahad wakiambatana na Gavana wa Benki Kuu na Waziri wa Fedha kupita mitaani Saudi na Magunia ya Dinari ama US$ wakigawa Fedha kwa wananchi, pia hivyo hivyo tusimlaumu Raisi Kikwete kwanini haambatani na Prof. Ndulu na Mama Saada Salum Mkuya na magunia na mabunda ya noti wakigawa fedha?,,,hiyo haiwezekani kwa kuwa kama Saudi Arabia tajiri wa mafuta hayo hayafanyiki na pia Tanzania kwa Kiwkete msitegemee fanyeni kazi ndio mpate fedha!!!
Hongera Raisi Jakaya Kikwete!!!