Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara
Tanzania (TanTrade), Bibi Jacqueline Mneney Maleko akipokea Kompyuta, Vifaa vya Ofisi na Samani kutoka kwa Mwakilishi wa Taasisi ya Marekani ya USAID - East Africa Trade Hub,Bw. Peter Nash. Vifaa hivi ni kwa
ajili ya kuanzisha rasmi Ofisi za Kamati za Ushirikiano Mipakani (Joint Border Committees)
zilizoanzishwa kwenye mipaka 7 ambayo ni Namanga, Kasumulu, Tunduma, Rusumo,
Kabanga, Mtukula na Sirari. Madhumuni yake ni kuimarisha ufanisi wa kupitisha mizigo
mipakani na kupata taarifa za biashara mipakani. Tukio hili lilifanyika tarehe 19 Agosti 2014
katika Uwanja wa Mwl. J.K.Nyerere Barabara ya Kilwa, Dar-es-Salaam. Wanaoshuhudia ni
Maafisa Waandamizi na Watendaji wa TanTrade. (Picha na TanTrade)
Home
Unlabelled
TanTrade yapokea vifaa kutoka Taasisi ya Marekani ya USAID
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Love you mummy for your hard work and integrity. Keep going you have all of our support. AMaleko
ReplyDelete