Na Rose Masaka,Maelezo 

 Tanzania imepokea mwongozo mpya juu ya Sheria na Kanuni zinazohusu haki za polisi kumweka mtuhumiwa chini ya ulinzi na kabla ya kesi kusikilizwa ili kuwapa uelewa wa kutosha wananchi juu ya haki zao za msingi.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana Katibu mtendaji wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Bi.Mary Massay amesema mtuhumiwa anatakiwa kumhoji polisi kosa gani amekamatwa nalo kabla ya kufikishwa kituoni.

Bi Massay alisema wananchi wengi wamekuwa hawafahamu haki zao za msingi pindi wanapokamatwa na polisi hivyo kupelekea kuishia magerezani kwa kukosa uelewa wa haki zao za msingi. Alisema mwongozo huo umepitishwa na Tume za Haki za Binadamu Tanzania, Zimbabwe, Malawi, Tunisia na Ivory Coast na unahusu utendaji wa polisi ambapo unawataka wananchi wa Tanzania kutambua haki zao za msingi pindi wanapokamatwa na polisi.

Akifungua mkutano huo mwandishi maalumu wa wafungwa na mazingira Kamishna Med Kaggwa kutoka taasisi ya Haki za Binadamu Uganda aliongeza kuwa Afrika inahitaji ushauri ili iweze kufanya kazi zake kwa ufanisi kwa sababu kuna maeneo mengi ya kisheria ambayo yanatakiwa kufanyiwa marekebisho.

Kamishna Kaggwa alisema mtuhumiwa kufungwa kabla ya uchunguzi kukamilika ni ukiukwaji wa sheria hivyo polisi wanatakiwa kufuata na kuheshimu sheria na kanuni zilizotungwa na nchi. Alisema kutokana na utafiti uliofanywa unaonyesha kuwa asilimia 41.3 ya wafungwa wa Afrika hukuo afrika kusini ikiwa na wafungwa wengi zaidi,na asilimia 50 ya wafungwa wa Tanzania ni wafungwa wa muda mchache kati ya miaka 3 hadi 4 kupata hukumu.
Mwandishi Maalumu wa Wafungwa Bw. Med Kaggwa kutoka Taasisi ya Haki za Binadamu ya Uganda aliyesimama akifungua Warsha ya siku mbili juu ya mwongozo mpya wa Sheria na Kanuni za polisi kumweka mtuhumiwa chini ya ulinzi na kabla ya kusikilizwa.warsha hiyo imefanyika jijini Dar es Salaam leo.
Bi. Louise Edward kutoka Taasisi ya “African Policing Civilian Oversight Forum (APCOF) akitoa mada katika Warsha ya siku mbili juu ya mwongozo mpya wa Sheria na Kanuni za polisi kumweka mtuhumiwa chini ya ulinzi na kabla ya kusikilizwa.warsha hiyo imefanyika jijini Dar es Salaam leo.
Washiriki wakiwa katika picha ya pamoja katika Warsha ya siku mbili juu ya mwongozo mpya wa Sheria na Kanuni za polisi kumweka mtuhumiwa chini ya ulinzi na kabla ya kusikilizwa.warsha hiyo imefanyika jijini Dar es Salaam leo. Picha zote na Benjamin Sawe wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini WHVUM

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. KWA UELEWA WANGU MTOA HAKI ANATAKIA ATOE HAKI HATA KABLA ANAYEPEWA HAKI HAJAIULIZIA. KWA HIYO POLISI WATOE HAKI YA RAIA HATA KAMA HUYO RAIA HAJUI HAKI YAKE. HAIMANIISHI KWAMBA MTU ASIPOJUA HAKI YAKE NDIYO ANYIMWE HAKI YAKE; HII SI KWELI. TUJITAHIDI WANANCHI WENZANGU KUTOA HAKI AMBAYO IKO CHINI YA USIMAMIZI WAKO KWA MHUSIKA HATA KABLA MHUSIKA HAJAIOMBA. KAZI NJEMA KAKA MICHUZI.

    ReplyDelete
  2. UKO SAHIHI SANA MKUU WANGU HAPO JUU....KAMA VILE AMBAVYO KUTOJUA SHERIA HAKUMPI "EXCUSE" ALIYETENDA KOSA....KADHALIKA KUTOJUA HAKI HAKUPASWI KUMFANYA ANAYEJUA HAKI ASIMPE ASIYEJUA HAKI, HAKI YAKE...TUKIUFIKIA UPEO HUO WA USTAARABU TAIFA LITAKUWA LINASHUHUDIA JAMII YA KISTAARABU SANA HAPA KWETU TZ.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...