SHIRIKA la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC) ni Shirika la Serikali ya Mapinduzi Zanzibar lililoanzishwa mwaka 1968 kwa madhumuni ya kununua na kuuza mazao ya wakulima kama vile karafuu, mbata, makonyo, pilipili hoho, makombe na mwani.

Shirika hilo tokea wakati huo wa miaka ya sitini limekuwa likitimiza wajibu huo na majukumu mengine  iliyopewa na Serikali kwa ufanisi na kwa uwazi ili kutoa huduma nzuri kwa wakulima na wauzaji wa mazao hayo ambayo kwa kiasi kikubwa yaliwapatia wananchi wa visiwani faida kubwa.
Visiwa vya Zanzibar ni visiwa vinavyosifika kwa uzalishaji wa zao la karafuu bora ambalo pia katika miaka mingi ya nyuma, vilitajika kwa uzalishaji wa kiwango cha juu cha karafuu duniani.


Wananchi wengi wakati huo walikuwa wakizithamini mno karafuu kutokana na umuhimu wake wa kuwapatia kipato, lakini, pia kama zao tegemezi la uchumi wa Zanzibar katika kupata fedha za kigeni kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wake.


Akizungumza na Zanzibar Leo katika mahojiano maalum ya mafanikio ya Shirika la Biashara la Taifa (ZSTC), Naibu Mkurugenzi Muendeshaji wa Shirika hilo, Jongo Suleiman Jongo, alisema, 
ZSTC imepitia katika hatua mbalimbali za mafanikio na changamoto tokea lilipoanzishwa mwaka 1968.

Alisema, ZSTC ilikuwa kila kitu katika uagizaji wa bidhaa za biashara na Shirika hilo tangu wakati huo wa miaka ya sitini, lilikuwa likitimiza wajibu huo na majukumu mengine  iliyopewa na Serikali kwa ufanisi na kwa uwazi ili kutoa huduma nzuri kwa wakulima na wauzaji wa mazao hayo ambayo kwa kiasi kikubwa yaliwapatia wananchi wa Zanzibar faida kubwa.

Alisema, katika miaka ya 1980-90, Shirika la ZSTC pamoja na kuwa lilikua likiendeleza majukumu hayo, lakini, pia Serikali kwa nia safi ilitoa nafasi kwa wananchi wake wenye uwezo wa kulima na kusafirisha mazao ya mbata, pilipili hoho, makombe na mwani kufanya hivyo ili kuongezea kipato chao. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...