Basi la Simba mtoto linalofanya safari zake kati ya Dar na Tanga likiwa limegongana uso kwa uso na Lori la mizigo katikati ya Daraja la Mto Wami mkoani Pwani,dereva wa lori hilo amefariki papo hapo na wengine kujeruhiwa.tutaendelea kupeana taarifa zaidi hapo baadae.
Baadhi ya wasamaria wema wakijaribu kumchomoa Dereva  wa Lori hilo aliyekuwa amebanwa vibaya,pichani ambalo namba zake za usajili hazikufahamika mara moja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 14 mpaka sasa

  1. Kwa haraka tu inawezekana hilo lori lilikatika break....otherwise madereva wote walikuwa wamekunywa au wana akili yao mbovu...

    ReplyDelete
  2. Mdau LubidaOctober 31, 2014

    Siyo rahisi kuamini kutokea kwa ajali kama hiyo hapo darajani. ni wazi kuna uzembe mkubwa wa madereva waliohusika na ajari hiyo. mahali kama hapo huwa panakuwa na speed ndogo kama 30km/h hivi ambayo haingeweza kusababisha ajari mbaya na kuua watu.

    ReplyDelete
  3. Hizi ajali zinatisha

    ReplyDelete
  4. Ila Tanzania kweli ee kweli. Inawezekanaje ajali itokee darajani jamani? kweli? sasa na daraja la kigamboni si ndio watu wataishia bahari ya hindi? mie nipo hapa. Anyway, pole sana majeruhi na waliofariki wapumzike kwa amani ya bwana. This is too much Tanzania.

    ReplyDelete
  5. Kawaida bongo,same stuff everyday

    ReplyDelete
  6. Madereva nendeni mukasomee udereva ili mujue sheria za barabara

    ReplyDelete
  7. Jamani hata siamini kilichotokea. Huu ni uzembe wa madereva kutokuwa makini na vyombo vya moto hadi kutokuwa na umakina kama wamebeba roho za watu...Embu ona sasa can you imagine? Yaani ....

    ReplyDelete
  8. hapo itakuwa umefanyika uzembe wa hali ya juu hawakutaka kusubiriana kwani hapo inaingia gari moja tuu.
    Nyingine inatakiwa kusubiri aonekweupe ndio aingie.

    ReplyDelete
  9. Kwakweli daraja la wami linabidi liongezwe upana kwani ni laenzi za wakoloni, inakuwa vigumu kwa magari makubwa kupishana

    ReplyDelete
  10. IVI KWELI KTK ULIMWENGU HUU TULIOKUA NAO SASA AJARI ZA KUGONGANA USO KWA USO ZIPO KWELI??KWELI TZ SOKOMOKO OVYOOOO YAANI SIPATI PICHA....HILI SI SUALA LA HAO WALIOPATA AJARI TU KUNA WENGI WANAINGIA HAPA....NI TAABU TUPU....

    ReplyDelete
  11. HII INAONYESHA JINSI WATU HAWAJALI UHAI WAO, KWASABABU HII NI AJALI AMBAYO IMETENGENEZWA MAKUSUDI, DARAJA LA WAMI HUWEZI KUKOSA KUMWONA MWENZIO ANAEKUJA MBELE YAKO ILIKUWAJE MPAKA UINGIE DARAJSANI WAKATI MWENZIO UNAMWONA AMESHAINGIA KWENYE HILO DARAJA JAMBAMBA NA WEWE UNAINGIA TU.

    ReplyDelete
  12. Waswahili tunasema: Ajali haina kinga!!! How dumb!

    ReplyDelete
  13. Ni bola daraja hili magufuri alitanue au viwekwe vizuizi vya kusubiliana mwazoni mwa daraja

    ReplyDelete
  14. Si sahihi kuyaita matukio haya Ajali. Haya ni mauaji ya barabarani.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...