Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Neema Muro, (Kushoto), akizungumza na baadhi ya wajumbe wa idara ya utumishi wa walimu, kwenye eneo la mradi wa nyumba za Mfuko huo eneo la Lukobe mjini Morogoro mwishoni mwa wiki. Wajumbe hao walifanya ziara hiyo mara baada yab kuhudhuria semina ya siku moja iliyoandaliwa na Mfuko huo kwa lengo la kuwaelimisha juu ya faida mwanachama anazoweza kupata anapojiunga na Mfuko huo.
Mkurugenzi wa uendeshaji wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Neema Muro, (Kushoto), akiwapa maelezo, baadhi ya wajumbe wa tume ya utumishi wa walimu, kuhusu mradi wa nyumba za Mfuko huo, zilizoko eneo la Lukobe mjini Morogoro, mwishoni mwa wiki.
Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Abdul Njaidi, (Mwenye T-Shirt), akiwapa maelezo wajumbe wa idara ya utumishi wa walimu, kuhusu nyumba za Mfuko huo zilizoko eneo la Lukobe mjini Morogoro, mwishoni mwa wiki mara baada ya kuhudhuria semina ya siku moja iliyoandaliwa na Mfuko huo mjini humo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...