Ofisa mwandamizi wa habari na mahusiano ya umma wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, Bw. Karimu Meshack (kushoto) akijadiliana jambo ndani chumba cha mapumziko cha wageni mashuhuri na Mwakilishi mkazi shirika la UNESCO nchini Bi. Zulmira Rodrigues pamoja na Afisa mipango kitaifa, kitengo cha Sayansi UNESCO,Tanzania, Gabriela Lucas kabla ya kuwasili kwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Getachew Engida.
Mwakilishi mkazi shirika la UNESCO nchini Bi. Zulmira Rodrigues akimlaki Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Getachew Engida wakati alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kwa ajili kuhudhuria mahafali ya pili ya Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela jijini Arusha yanayofanyika kesho. Kulia ni Ofisa mwandamizi wa habari na mahusiano ya umma wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, Bw. Karimu Meshack na wa pili Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO, Dr. Moshi Kimizi.
Mwakilishi mkazi shirika la UNESCO nchini Bi. Zulmira Rodrigues (katikati) akimlaki kwa furaha Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Getachew Engida (kushoto) aliyewasili jioni hii jijini Arusha na shirika la ndege la Ethiopia. Kulia ni Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO, Dr. Moshi Kimizi.
Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Getachew Engida akisalimiana na Ofisa mwandamizi wa habari na mahusiano ya umma wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, Bw. Karimu Meshack kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).
Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Getachew Engida akiwa na mwenyeji wake Mwakilishi mkazi shirika la UNESCO nchini Bi. Zulmira Rodrigues mara baada ya kuwasili wakielekea kwenye chumba cha mapumziko cha wageni mashuhuri.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...