Wadhamini wakuu wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara,Kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania imetangaza rasmi zawadi zitakazotolewa hivi karibuni kwa Mabingwa wa ligi hiyo iliyomalizika hivi karibuni ambapo timu ya Yanga yenye makazi yake Jangwani jijini Dar es Salaam iliibuka na ubingwa.
Kwa mujibu wa mkataba wa ligi na mdhamini mbali na zawadi kutolewa  kwa timu bingwa zimekuwa zikitolewa pia kwa,mshindi wa pili na wa tatu katika ligi,mfungaji bora,timu iliyoonyesha nidhamu,mchezaji bora wa mwezi na wa ligi nzima,refa bora , kocha bora na golikipa bora.
Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu amethibitisha kuwa fungu nono litakalokabidhiwa kwa mabingwa na ambapo  alisema kimeongezeka kiasi cha milioni 13 tofauti na mkataba wa awali.
“Kama inavyojulikana kuwa thamani ya shilingi imeshuka hivyo kama wadhamini tumelazimika kuongeza fedha za zawadi ili ziendane na wakati na lengo kubwa  ni kuongeza motisha kwenye ligi hii kubwa ya soka nchini ambayo kwa miaka kadhaa imekuwa ikidhaminiwa na kampuni ya Vodacom”.
 Alizitaja zawadi  timu bingwa itapata shilingi 80,401,160/- tofauti na 75,565,000/- za awali,mshindi wa pili shilingi  40,200,580/- awali zilikuwa 37,782,500/-,mshindi wa tatu shilingi  28,714,700/- awali zilikuwa shilingi 26,987,5000/-,mshindi wa nne shilingi 22,971,760 awali zilikuwa shilingi 21,590,000/-,mfungaji bora shilingi 5,742,940/- ambapo awali ilikuwa 5,397,500/-,golikipa bora shilingi 5,742,940/- awali ilikuwa shilingi 5,397,500/-,timu iliyoongoza kwa nidhamu bora shilingi 17,228,820/- awali ilikuwa 16,192,500/-,Mchezaji bora wa msimu wa 2014/2015 shilingi 5,742,940/- ambapo awali ilikuwa 5,397,500/-,Refa bora shilingi 8,614,410/- awali ilikuwa 8,096,250/-na kocha bora shilingi 8,614,410/- ambapo awali ilikuwa 8,096,250/-pia kuna zawadi ya milioni 9,000,000/- ambapo kila mchezaji bora wa mwezi alikuwa akizawadiwa milioni 1,000,000/katika kipindi cha miaka 9
Alisema baada ya kumalizika ligi mchakato unafanyika wa kukabidi zawadi katika siku za karibu. “Katika siku chache zijazo tutawakabidhi washindi na wadau wote waliofanya vizuri na tunajivunia kuona ligi hii inazidi kuwa na msisimko mwaka hadi mwaka”.
Alipoulizwa  mipango ya kampuni   iwapo itaendelea kudhamini ligi hiyo alisema ninapenda kuwahakikishia wapenzi wa soka nchini wasiwe na wasiwasi kuhusiana na suala la sisi kuendelea kuwa wadhamini kwani kwasasa bado tupo mezani kwa mazungumzo ya kina na TFF  kujua nini tukiboreshe kwa msimu ujao na wapi tulikokosea msimu huu uliopita  kwa kifupi hakuna kitakachoharibika muda ukifika tutawajulisha,Alisema Nkurlu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...