Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake kwa mwaka 2015/2016 bungeni leo mjini Dodoma. Mabalozi wa Tanzania kwenye nchi mbalimbali duniani wakifuatilia bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa mwaka 2015/2016 iliyowasilishwa leo bungeni mjini Dodoma. Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Harrison Mwakyembe akimsikiliza kwa makini mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe. Makongoro Nyerere (kushoto) nje ya ukumbi wa bunge leo mjini Dodoma. Kulia ni mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe. ShyRose Bhanji. Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju (kulia) akisisitiza jambo kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (katikati) kwenye viwanja vya bunge mjini Dodoma jana. Waziri
wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Harrison Mwakyembe akifurahia jambo na
wabunge wa bunge la Afrika Mashariki Mhe. Makongoro Nyerere (kushoto) na Mhe.
ShyRose Bhanji (kulia) mara baada ya kuwasilisha bajeti ya wizara yake kwa
mwaka 2015/2016 leo bungeni mjini
Dodoma. PICHA ZOTE NA FATMA SALUM - MAELEZO.
Home
Unlabelled
WIZARA YA MAMBO YA NJE NA WIZARA YA USHIRIKIANO AFRIKA MASHARIKI ZALENGA KUBORESHA UHUSIANO WA TANZANIA KIMATAIFA.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...