Klabu ya Kimondo Super Sports inayoshiriki ligi daraja la kwanza Tanzania yenye maskani yake wilayani Mbozi mkoani Mbeya inapenda kutoa tamko juu ya mkanganganyiko wa taarifa za kuptosha za usajili wa mchezaji wake Geofrey Bahati Mwashiuya.

Klabu inasikitishwa saana na habari/taarifa zenye mkanganyiko zinazotolewa na msemaji wa timu ya Yanga,Katibu wa timu ya Yanga na mchezaji wetu Geofrey Mwashiuya katika vyombo mbalimbali vya habari;
Jerry Muro alisikika katika vyombo vya habari akijinadi kuwa klabu ya soka ya Yanga imemsajili Geofrey Mwashiuya tangu Oktoba,2014 kwa kandarasi ya miaka mitatu,wakati huohuo Katibu wa Yanga Dkt,Jonas Tiboroha alidai mchezaji huyu alisajiliwa na klabu ya Yanga tangu mwezi Februari,2015.
Klabu ya KIMONDO inasikitishwa na taarifa hizi zenye mkanganyiko mkubwa kuhusu suala la mchezaji huyu,na kwa kauli hizo mbili zinazokinzana Watanzania wanaweza kuona ukweli wa mambo ukoje.

Taarifa sahihi ni kwamba mchezaji Geofrey Mwashiuya ana mkataba wa miaka minne na timu yetu ya KIMONDO  na ndio muda sahihi ulioandikwa katika TMS na uliopo katika mkataba wa maandishi. Zaidi klabu ya KIMONDO inasikitishwa na taarifa hizi za upotoshwaji zinazofanywa na YANGA kwa makusudi kabisa kuwa mchezaji wetu hana mkataba na sisi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 06, 2015

    Kuchia suala hili likakua namna hii ni fedheha kwa klabu ya Yanga ambayo inasajili wachezaji wa kimataifa kwa mamilioni. Ni bora kuongea na KIMONDO na kumnunua mchezaji ili marumbano yaishe, nina hakika gharama yake haiwezi kufikia hata robo ya mchezaji yeyote kutoka nje ya nchi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...