Kwa kuzingatia marekebisho ya Kanuni ya Ligi Daraja la Pili (SDL) yaliyofanywa na Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) hivi karibuni, SDL kwa msimu wa 2015/2016 itachezwa katika makundi manne ya timu sita sita kwa mtindo wa nyumbani na ugenini.

Timu itakayoongoza kundi itacheza Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu wa 2016/2017 wakati ya mwisho katika kila kundi itarudi kucheza Ligi ya Mkoa wake kwa msimu wa 2016/2017. 
Makundi ya SDL ni kama ifuatavyo; Kundi A ni Abajalo FC (Tabora), Singida United (Singida), Mvuvuma FC (Kigoma), Milambo FC (Tabora), Green Warriors (Dar es Salaam) na Transit Camp (Dar es Salaam).
Timu zinazounda kundi B ni Bulyanhulu FC (Shinyanga), JKT Rwamkoma (Mara), Pamba FC (Mwanza), AFC Arusha, Madini FC (Arusha) na Alliance Schools (Mwanza).
Kundi C ni Kariakoo (Lindi), Mshikamano FC (Dar es Salaam), Cosmopolitan (Dar es Salaam), Abajalo FC (Dar es Salaam), Changanyikeni Rangers (Dar es Salaam) na Villa Squad (Dar es Salaam).
Nazo African Wanderers (Iringa), Mkamba Rangers (Morogoro), Town Small Boys (Ruvuma), Wenda FC (Mbeya), Coca-Cola Kwanza FC (Mbeya) na Sabasaba United (Morogoro) zitakuwa kundi D. 
Klabu nyingi bado hazijatuma jina la uwanja wa nyumbani, hivyo zinakumbushwa kufanya hivyo haraka ili kurahisisha upangaji wa ratiba. 
Ligi Daraja la Pili (SDL) msimu wa 2015/2016 inatarajia kuanza Oktoba 17 mwaka huu.

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA 
WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa


  1. Duuhh,,nimeshangaa kuona iliyowahi kuwa miamba ya soka Tanzania,,imeshuka kutoka kucheza ligi kuu mpaka daraja la 2? Timu yangu ya Arusha FC, pAMBA YA mWANZA, Vila Aquad, Kariakoo Lindi, duu hatari..

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...