Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe.Dkt. Harrison Mwakyembe (Mb.) akifungua Mkutano wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Afrika Mashariki ambao pamoja na mambo mengine utapokea na kujadili taarifa ya ziara ya Mawaziri nchini Burundi kuhusu hali ya kisisasa nchini humo. Mkutano huo ambao ni maandalizi ya Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi utakaofanyika tarehe 06 Julai, 2015, umefanyika kwenye Hoteli ya Serena, Jijini Dar es Salaam tarehe 05 Julai, 2015.
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) Dkt. Richard Sezibera naye akizungumza wakati wa mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Afrika Mashariki
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula (kulia) akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Joyce Mapunjo wakifuatilia kwa makini ufunguzi wa Mkutano wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Afrika Mashariki uliokuwa ukiendelea katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam
Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa nao wakifuatilia kwa makini ufunguzi wa Mkutano huo.
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...