Dkt Gideon Shoo (mwenye gwanda la buluu) mwanahabari mwandamizi na mkongwe akielezea  alivyoamua kuingia katika kilimo hai cha kisasa alipotembelewa shambani na nyumbani kwake kata ya Kerege wilaya ya   Bagamoyo mkoa wa Pwani na maofisa kutoka Envirocare , asasi isiyokuwa ya kiserikali inayojihusisha na mazingira na  haki za binadamu. 
 Dkt Gideon Shoo akionesha anavyozalisha mbolea ya samadi
 Dkt Gideon Shoo akitembeza wageni kwenye shamba lake sehemu ya mbogamboga.

Ni jambo la kawaida kwa mtu yeyote ajira yake inapokaribia kufikia ukomo hufikiria namna atakavyoondesha maisha yake kwa kutafuta shughui itakayo mfanya aweze kujiingizia kipato kwa ajili yake na famiia kwa ujumla.
Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa Dkt.  Gideon Shoo, mwanahabari mwandamizi na mkongwe ambaye  aliamua kuingia katika kilimo hai cha kisasa  ambacho hakitumii dawa za kemikali kutoka viwandani .
Dakta Shoo kwa sasa kilimo hicho anakifanya nyumbani kwenye shamba katika kata ya Kerege wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani.


Akizungumza wakati alipotembelewa shambani na nyumbani kwake  na maofisa kutoka Envirocare , asasi isiyokuwa ya kiserikali inayojihusisha na mazingira , hakiza binadamu alisema kilichomhamisha kuingia kwenye shughuli hiyo ni kutokana na kukulia kwenye kilimo. 



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...