Mwenyekiti wa Mtandao wa Kimataifa wa Wabunge (PGA) Mhe. Pindi Chana ( MB) akimkabidhi Rais wa Baraza Kuu la 70 la Umoja wa Mataifa, Bw.Mogens Lykketoft,Tamko la wabunge lenye sahihi 607 za wabunge kutoka mataifa 70 la kutokomeza ndo za utotoni na za kulazimisha katika hafla fupi iliyofanyika Umoja wa Mataifa siku ya Jumatatu.
Mwakilishi wa Kudumu wa Zambia katika Umoja wa Mataifa, Balozi Dr. Mwaba Kasese-Bota akizungumza wakati wa hafla hiyo ambapo alianisha mipango mbalimbali inayofanywa na serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wakiwamo viongozi wa kimila katika kuzunguia ndoa za utotoni na za kulazimishwa.
Na Mwandishi Maalum, New York
Mtandao
wa Kimataifa wa Wabunge kutoka Mabunge mbalimbali Duniani (PGA), umemkabidhi Rais wa Baraza Kuu la 70 la Umoja wa Mataifa Bw. Mogens
Lykketoft, tamko la kukomesha ndoa za utotoni na za kulazimishwa kwa watoto wa kike.
Akikabidhi
tamko hilo lenye sahini Zaidi ya 607 kutoka nchi 70 Mwenyekiti wa Mtandao huo wa wabunge, Mhe. Pindi Chana na ambaye pia ni Naibu Waziri
wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto amesema, kukabidhiwa kwa tamko hilo kwa
Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa
kunakwenda sambamba na
maadhimisho ya siku ya mtoto wa
kike ambayo huadhamishwa kila Octoba ya mwaka.
Mwenyekiti
wa PGA, amesema wakati wa hafla hiyo fupi iliyofanyika hapa Umoja wa Mataifa, siku ya Jumatatu
kwamba, ushirikiano wa wadau mbalimbali
hasa wabunge , serikali na asasi za
kiraia ni muhimu sana ikiwa jumuiya ya
kimataifa inataka kuondokana na kumaliza
tatizo la ndoa za utotoni na za kulazimishwa.
Hongera sana na pongezi za dhati Bi Ellen Maduhu kutuwakilisha, pia pongezi za dhati kwa washiriki wote. Ni kweli kabisa imefikia wakati sasa lazima kuwepo na mikakati thabiti na sheria imara za kumlinda, kumtetea na kumsaidia kwa kila hali mtoto wa kike na kulitokomezea mbali suala zima la ndioa za utotoni na hata za kulazimishwa pasina ridhaa yake, kwani vitendo hivyo vimekuwa vikimnyima fursa na nafasi mbali mbali katika kujiendeleza kielimu, kimaendeleo na katika fani nyingine mbali mbali ambazo zingeweza kumkombowa katika maisha yake ya baadae na badala yake kujikuta yupo katika ndoa asizozitarajia katika umri mdogo kabisa na pengine kwa kulazimishwa bila kutaka au kukubali kwa ridhaa yake.
ReplyDelete