Meneja Biashara kutoka shirika la Mzinga Morogoro Pingu Kamenyi akiwaeleza wandishi wa habari leo jijini Dar es salaam (hawapo pichani) kuhusu mafanikio ya Shirika hilo katika kipindi cha Miaka kumi ya Serikali ya awamu ya nne ikiwemo uzalishaji wa zana bora  za kilimo na ujenzi zinazolenga kuwainua wajasiriamali wadogo ili waweze kuinua uchumi wao na wa taifa kwa ujumla.  Wa pili kushoto ni Msemaji wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Luteni Kanali Juma Nkangaa Sipe na wa kwanza kushoto ni Afisa Habari wa Idara ya Habari (MAELEZO) Frank Mvungi.
 Msemaji wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Luteni Kanali Juma Nkangaa Sipe akitoa wito kwa watanzania kutumia bidhaa zinazozalishwa na Shirika la Mzingira ambalo ni moja ya Taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa  leo jijini Dar es salaam. Wa pili kulia ni Meneja Biashara kutoka shirika la Mzinga Morogoro Pingu Kamenyi.
 Miundo mbinu ya umwagiliaji katika shamba la mpunga.
Frank Mvungi-MAELEZO
Serikali kupita Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa imeendelea kuwainua wananchi kupitia shirika la Mzinga kwa kuzalisha zana za kilimo, ufugaji na Ujenzi zitakazosaidia kukuza na kuongeza kasi ya uzalishaji wenye tija katika sekta hizo.

Hayo yamesemwa na Meneja biashara wa Shirika hilo jana jijini Dar es salaam Bw. Pingu Kamenyi wakati wa mkutano na wandishi wa habari uliolenga kueleza mafanikio ya shirika hilo katika kipindi cha miaka kumi ya Serikali ya Awamu ya Nne.

Akifafanua Kamenyi amesema  Serikali imepata mafanikio makubwa  kupitia shirika hilo kwa  kutekeleza miradi mbalimbali kama vile Ujenzi wa daraja la Mabwepande wilaya ya Kinondoni Dar es Salaam, Ujenzi wa nyumba za Halmashauri ya Masasi mkoani Mtwara, Ujenzi wa jengo la utawala la Hospitali ya Wilaya ya Morogoro na Ujenzi wa uzio wa Halmashauri ya Manispaa hiyo.

“Shirika la Mzinga lilianzishwa kwa lengo la kuwasaidia wananchi ili waweze kujikomboa kiuchumi ndiyo sababu iliyopelekea kuanzishwa kwa kampuni Tanzu ya Mzinga inayotekeleza miradi kama vile ya ujenzi. “Alisisitiza Kamenyi.

Shirika limekuwa na ushirikiano mzuri katika kutekeleza majukumu yake kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali nchini.

Baadhi ya taasisi hizo zinajishughulisha na utafiti na maendeleo ni hapa nchini ni pamoja COSTECH, CoET, CAMARTECTIRDO lengo likiwa kupata teknolojia za kurahisisha utendaji kazi katika shughuli mbalimbali zinazolenga kuwainua wananchi kiuchumi.

Katika jitihada za kupanua huduma zake, Kamenyi amebainisha kuwa shirika hilo limefungua vituo  vya kuuza milipuko, silaha na risasi za kiraia, na pia wameweza kufungua vituo vinne zaidi vya mauzo katika miji ya  Mererani , Arusha  , Shinyanga  na Mpanda.
Kusoma zaidi na KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...