Na  Bashir  Yakub
Hatua  unazopitia  unapohitaji  hatimiliki  ni  tofauti  na  hatua  unazopitia  unapohitaji  kubadilisha  jina  katika  hatimiliki( transfer). Kutafuta  hati  na  kubadilisha  hati  ni  michakato  miwili  tofauti.  Makala  kadhaa  zilizowahi  kuandaliwa zilieleza  namna  ya  kubadilsha  hati  na  sio  namna  ya kutafuta  hati  mpya. Makala  ya  leo  yanaeleza  namna  ya  kupata  hati  mpya.

1.TOFAUTI  YA  KUTAFUTA  HATI NA  KUBADILISHA  HATI.
Unapotafuta  hati  maana  yake  ni  kuwa  ardhi  yako  haikuwa  na  hati  kabisa  na  sasa unaanza  mwanzo  kabisa kutafuta. Kwa wamiliki  wa  ardhi  za  namna  hii  mara  nyingi  ni  zile  ardhi  zenye  mikataba  ya  kununulia(  sale  agreement),ardhi zenye  barua  ya  toleo( letter  of  offer), na  nyingine  zinakuwa  hazina  waraka  wowote.  Kwa ardhi  za  namna  hii unaposema  unahitaji  hati  ni  lazima  uanze  mwanzo  kabisa.
Aidha  kubadilisha  hati  maana  yake ni  kuwa,  hati  inakuwepo  isipokuwa  inabadilishwa  kutoka  jina  moja  kwenda  jingine. 
Pengine  ni  muamala  wa  mauziano  kwahiyo  jina  linatoka  kwa  muuzaji  kwenda  kwa  mnunuzi  au  linatoka  kwa  marehemu  kwenda  kwa  msimamizi  wa  mirathi. Kwahiyo  kubadilisha  ni  kubadilisha  tu  na  wala  sio  kutafuta  hati  mpya.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...