Baada ya jana kuiripoti habari ya lile dampo haramu la temeke mwisho, sasa kijipu upele kilichokuwa kikisumbua na kukera watu wa Temeke Mwisho, Kimetumbuka kabla hata ya kupakwa kitunguu swaumu. Lile dampo korofi limesafishwa usiku mzima wa kuamkia leo, na hali sasa ni kama unavyoiona katika picha.
Somo hapa ni kwamba;
1. Tusifanye kazi kwa mazoea, mpaka watu walalamike baada ya kudhurika- reactive mode
2. Kama uwezo wa kusafisha uchafu ule kwa usiku mmoja upo, kwa nini msingefanya hayo tangia siku za nyuma
SISI WAKAZI WA KARIBU NA ENEO HILI, TUNAOMBA DAMPO HILI LIONDOLEWE HAPA, NA KIWANJA HIKI CHA WAZI KILICHOVAMIWA WARUDISHIWE VIJANA WETU WA TEMEKE WAENDELEE KUKITUMIA KWA MATUMIZI CHANYA.
Najua wahusika mnaisoma Globu hii ya Jamii na suala hili linaloharibu mandhari nzuri ya temeke mwisho mtalifanyia kazi.
Malori yakipishana kuondoa uchafu uliokuwa umerundikwa kwenye dampo hilo.
I can only say one word here:impressive
ReplyDelete