Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Simon Sirro, akizungumza na baadhi ya Mashabiki wa Yanga waliokuwa wamekusanyika nje ya Geti Kuu la Uwanja wa Taifa, kuwataka kutawanyika kurudi makwao kutoka na Uwingi wa washabiki waliokuwepo uwanjani hivi sasa, Kufuatia Mtanange baina ya Yanga na TP Mazembe ya Nchini Congo ikiwa ni muendelezo wa Mashindano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika. Kamanda Sirro amewataka Washabiki hao pamoja na wale wanaoendelea kuja Uwanja wa Taifa, kuahirisha safari hiyo kwani Uwanja umeshajaa, hivyo warudi tu majumbani kwani mchezo huo utaonyeshwa pia kupitia Vituo vya Televisheni.
 Kamanda Sirro akimtaka mmoja wa Washabiki hao kuacha fujo.
 Washabiki wa Yanga wakiwa nje ya Geti kuu la Uwanja wa Taifa.
Askari Polisi wakiwatawanya washabiki hao.
 Mshike mshike nje ya Uwanja wa Taifa kwa wale waliokaidi amri ya Jeshi la Polisi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...