Mkimbiza Mwenge wa Uhuru kitaifa akiwaongoza Askari wa Kikosi cha Kutulia Ghasia(FFU)kuingia katika halmashauri ya wilaya ya Arusha DC baada ya kumaliza mbizo zake halmashauri ya wilaya ya Meru zote zikiwa katika wilaya ya Arumeru mkoa wa Arusha .

Kiongozi wa Mbio za Mwenge kitaifa mwaka 2016,George Mbijima akisalimiana na watumishi wa halmashauri ya wilaya ya Arusha DC kabla ya kuanza kuweka Mawe ya Msingi na kuzindua miradi yenye thamani ya zaidi ya Sh 3 bilioni.

Mkurugenzi wa New Age Company Ltd,Godson Ngomuo akimwonyesha Samani zinazotengenezwa na kuuzwa na kampuni yake na kusaidia kutengeneza ajira kwa vijana wazawa.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge kitaifa mwaka 2016,George Mbijimaakizungumza na maafisa wa taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa wilaya ya Arumeru wanaotoa elimu dhidi ya Rushwa.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge kitaifa mwaka 2016,George Mbijima  akijiandaa kukabidhi hundi yenye thamani ya Sh 3 milioni kwa kikundi cha Vijana waliopata mikopo yenye riba nafuu,kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Arumeru,Alexander Mnyeti.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge kitaifa mwaka 2016,George Mbijima akiwakabidhi  hundi yenye thamani ya Sh 3 milioni kikundi cha Wanawake  waliopata mikopo yenye riba nafuu,kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Arumeru,Alexander Mnyeti.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...