Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa tume ya taifa ya Matumizi Bora ya Ardhi Dkt Stephen Nindi ( Kulia ), akikabidhi Mpango wa miaka 20 wa Matumizi Bora ya Ardhi wa Watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga, Mpango huo umelenga kutunza mazingira na Bio anuai Zilizopo nchini pamoja na kumnufaish Mwananchi wa Kipato cha kawaida.
Kiongozi wa Urasimishaji kupitia Programu ya LTSP, iliyo Chini ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi SAGWILE MSANANGA akitoa maelezo kuhusu Mradi wa kuwezesha Umilikishaji Ardhi kwa Wananchi pamoja na Vijiji Vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga Mkoani MOROGORO.
Mratibu wa Programu ya Kuwezesha Umilikishaji Ardhi katika Wilaya za MALINYI, KILOMBERO na ULANG, Godfrey Machabe aliyevaa Tai Shingoni, akimsikiliza kwa Umakini Kiongozi wa Urasimishaji ndugu Sagwile Msananga alipokuwa akielezea kuhusu Programu ya LTSP, kwa Washiriki wa Mafunzo ya Kuwezesha Umilikishaji wa Ardhi katika Wilaya ya Ulanga Mkoani MOROGORO.
Kaimu kamishna wa Ardhi nchini Bi Mary Makondo ( katikati), akimsikiliza Katibu tawala wa Wilaya ya ULANGA mkoani Morogoro Ndugu Abraham Mwaivile aliyevaa Koti la Rangi ya Kijivu akisisitiza Jambo kwa Washiriki wa mafunzo ya kuwezesha Umilikishaji Ardhi katika Halmashauri hiyo, ambapo zoezi la Upimaji Mipaka ya Vijiji na Utoaji hatimiliki za Ardhi litafanyika.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...