Kiwanja cha ndege cha Dodoma, sasa kinauwezo wa kupokea ndege zenye uwezo wa kubeba abiria 90, baada ya kurefushwa kwa barabara ya kutua na kuruka kwa ndege kwa kilometa 2.5.

Ndege ya Shirika la ndege la Tanzania (ATCL), leo ikitua kwenye kiwanja cha ndege cha Dodoma ikitokea mkoani Kigoma.
Mizigo ya abiria wa ndege ya shirika la ndege Tanzania (ATCL), ikiwa ndani ya gari la kampuni inayotoa huduma ya mizigo ya National Aviation Services (NAS), kwenye Kiwanja cha ndege cha Dodoma.
Mkuu wa Dodoma (kushoto) Mhe. Jordan Rugimbana akielekea kupanda ya ATCL akiwa ni mmoja wa abiria akitokea kwenye Kiwanja cha ndege cha Dodoma na kuelekea Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA). Kulia ni Meneja wa kiwanja hicho, Bw. Julius Mlungwana.
Mkuu wa mkoa wa Dodoma, Mhe. Jordan Rugimbana (kulia) akiagana na Meneja wa Kiwanja cha Ndege cha Dodoma, Bw. Julius Mlungwana kabla ya kupanda ndege ATCL, akielekea Jijini Dar es Salaam, leo.
Wanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya sekondari ya Uwela ya kitongoji cha Kikuyu mkoani Dodoma wakiwa katika ziara ya mafunzo kwenye Kiwanja cha ndege cha Dodoma, leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...