Mkuu wa Utawala wa Jeshi la Polisi (DCP) Leonard Paulo (katikati), akiwa
ameongozana na Naibu Kamishna wa Polisi mstaafu (DCP) Venance Tossi
(Kushoto) na Mkuu wa chuo cha Polisi Kidatu kilichopo mkoani Morogoro,
kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Zarau Mpangule, wakati alipowasili katika chuo
hicho kwa ajili ya kufunga mafunzo ya Utayari ya kuwajengea uwezo askari wakati
wanapotekeleza majukumu yao. Picha na Jeshi la Polisi.
Naibu Kamishna wa Polisi mstaafu (DCP) Venance Tossi (Kushoto), akizungumza
jambo na Mkuu wa Utawala wa Jeshi la Polisi (DCP) Leonard Paulo (katikati),
muda mfupi kabla ya kufunga mafunzo ya Utayari ya kuwajengea uwezo askari
wakati wanapotekeleza majukumu yao ya kazi za Polisi. Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Utawala wa Jeshi la Polisi (DCP) Leonard Paulo, akifanya mazoezi ya
viungo na baadhi ya askari wanaoshiriki Mafunzo ya Utayari na kujengewa uwezo
wakati wanapotekeleza majukumu yao ya kazi za Polisi, mafunzo yanayofanyika
katika Chuo cha Polisi Kidatu Kilichopo mkoani Morogoro. Picha na Jeshi la Polisi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...