Marehemu Mohamed Idi Mturuma aka Muddy enzi za uhai wake.

Umoja wa Wa Watanzania Ujerumani kwa ushirikiano na watanzania wanaoishi England na Spain kwa masikitiko makubwa sana tulipata msiba wa ndugu yetu mtanzania mwenzetu mcheza sarakasi Mohamed Idi Mturuma aliekuwa akiishi koloni Ujerumani na kufariki nchini spain alikokwenda kikazi.

Aliaga dunia tarehe 19.09.17 Kwa ushirikiano wa Watanzania wanaoishi nchi hizo tumeazimia kufanya kila liwezekanalo ili kuweza kusafisrisha mwili wa Marehemu ndugu yetu Mohamed Idi Mturuma kwenda kuzikwa nyumbani Tanzania Umoja wa Watanzania Ujerumani (UTU.e.V ) Unawatangazia watanzania wote wanaoishi popote pale Duniani kuunga mkono azma yetu kwa kutoa michango ya hali na mali ili tumsafirishe mwenzetu.

Shukran nyingi kwa msanii Mussa FAB Moses Kutoka England ambaye alisafiri mara baada ya msiba kutokea kwenda Spain kwa ajili ya kusaidia mchakato wa kuandaa kusafirisha mwili wa marehemu. Mussa Fab Moses anategemea kusafiri na mwili wa Merehem kwenda Tanzania kwa Mazishi

Watanzania wanaoishi England mnaweza kuwasiliana moja kwa moja na Saidi Kanda ili kuwasilisha michango yenu namba ya kiganjani +447404066607

Watanzania wanaoishi Tanzania mnaweza kuwasiliana na Eddy Sengo ili kuwasilisha michango yenu namba ya kiganjani +255656210725

Watanzania wanaoishi Ujerumani mnaweza kuwasiliana na Makamo mwenyekiti wa Umoja wa Watanzania Ujerumani (UTUe.V) Malumbo Salim Malumbo namba ya simu +49 1522 4082848

Mwili wa Marehemu ulisaliwa msikitini siku ya ijumaa iliyopita tarehe 22.09.17 na kupelekewa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti kwa ajili ya kusubiria safari.

UMOJA NI NGUVU; PENYENIA PANA NJIA; TUKITAKA TUTAWEZA KWA KUDRAZA MWENYEZIMUNGU INSHALLAH WABILAHI TAWFIQ

UMOJA WA WATANZANIA UJERUMANI (UTU e.V)
 Waumini wa kiisalam nchini spain wakijiandaa kuusalia mwili wa marehem Mohamedi Idi Mturuma nchi spain.
 Waumini wakiislam wakielekea msikitini kuusalia mwili wa marehemu Mohamedi Idd Mturuma.
baadhi ya marafiki  zake marehemu Mohamedi Idi Mturuma baada ya kutoka kuusalia mwili wa marehemu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...