Mmoja wa askari waliokuwa wamepangwa katika suala zima la kusimamia usalama ndani ya tamasha la Fiesta 2014 akihakikisha usalama wa kutosha unakuwepo katika eneo hilo,na watazamaji wanapata burudani iliyokusudiwa kutoka kwa wasanii mbalimbali waliotumbuiza usiku wa kuamkia leo katika tamasha la Fiesta 2014 lililofanyika usiku wa kuamkia leo katika viwanja vya Lidaz Kinondoni jijini Dar.
Shaa na madansa wake wakilishambulia jukwaa. 
Pichani kulia ni Msanii kutoka nchini Nigeria ajulikanae kwa jina la Kisanii Davido sambamba na Diamond Platnum kwa pamoja wakilishambulia jukwaa la fiesta 2014 usiku wa kuamkia leo.
Msanii kutoka THT,Barnaba akiimba wimbo wake wa Wahalade sambamba na madansa wake kwenye jukwaa la fiesta 2014,katika viwanja vya Lidaz Kinondoni jijini Dar.
Sehemu ya  umati wa watu waliokuwa wakishuhudia yaliyokuwa yakijiri kwenye jukwaa la Fiesta usiku wa kuamkia leo katika viwanja vya Lidaz Kinondoni jijini Dar.
Ilikuwa ni shoo moja nzuri kutoka nyumba ya vipaji ya THT
Pichani msanii Linah (nyeupe) akiwa na skwadi lake mara baada kumaliza kulishambulia jukwaa kwa pamoja.
Anaitwa Ally kiba ambaye inaelezwa kutoka kwa mashabiki  kuwa alifanyo shoo nzuri na iliyowavutia,na kuthibitisha uwezo wake kuwa ni kweli amerejea kwenye kiti chake cha usanii.
  Msanii kutoka nchini Marekani Clifford Haris a.k.a T.I akilishambulia jukwaa la Fiesta vilivyo
 Msanii kutoka nchini Marekani T.I akiwaimbisha mashabiki wake

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Davido alikuwepo eehhh...nasubiri kuona meno ya Mahakama baada ya amri yake kukiukwa

    ReplyDelete
  2. Kwani unadhani Bongo kuna sheria? Ukiwa nazo zaidi ya mwenzako basi we unapeta tu! Na sheria inakuwa msumeno kwa wasio nacho!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...