Taasisi ya Vodafone Foundation leo
imetangaza kuwa mpango wake wa kutoa elimu kidigitali umewezesha jamii zinazoishi
kwenye mazingira magumu yanayosababishwa na majanga mbalimbali na kujikuta zikiishi kwenye kambi za wakimbizi
kuweza kupata elimu.
Mpango
huu wa unatekelezwa katika maeneo yenye mazingira magumu ambako kuna
matatizo ya kutokuwepo nishati ya umeme na
upatikanaji wa mawasiliano hususani ya mtandao wa interneti na umeweza
kutekelezwa kwa ushirikiano na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia
Wakimbizi (UNHCR).
Ufunguzi
wa madarasa chini ya mpango huu unafanyika kwa kutumia masanduku maalum
yanayobeba vifaa vya kufundishia ,kuzalisha nishati ya umeme,kuchaji vifaa vya
kufundishia na modemu maalumu za interneti ambazo hazihitaji kuunganishwa papo
kwa papo .Vifaa vyote hivi vilivyoandaliwa kwa ajili ya mpango huu unaoendeshwa kwenye maeneo yenye mazingira
magumu vikiunganishwa kwa muda mfupi vinawezesha walimu maalumu walioandaliwa
kuvitumia kuweza kuwapatia elimu wanafunzi bila matatizo yoyote.
Masanduku maalumu ya kubeba vifaa vinavyotumika kutolea
elimu hili yameandaliwa kutumika kuchaji vifaa vyote na vikishawekwa kwenye
chaji kwa muda wa kati ya masaa 6-8 sanduku linaweza kutumika siku nzima
kufundishia bila kuhitaji nishati ya umeme.
Mpaka
mwaka ujao mpango huu utakuwa umetekelezwa katika shule 12 kwenye makambi ya
wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya,Nyarugusu nchini Tanzania na Demokrasia ya
Congo na utatoa elimu bora kwa watoto wapatao 15,000 wenye umri kati ya miaka 7
-20 .
Mpango
huu tayari umeonyesha mafanikio makubwa ambapo mnamo mwaka 2014 taasisi ya
Vodafone Foundation kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la
Kuhudumia Wakimbizi la UNHCR limeweza kutoa elimu kwa watoto wapatao 18,000
kwenye kambi ya Dadaab nchini Kenya na walimu waliokuwa wanaendesha mafunzo
chini ya mpango huu wanakiri kwamba
umeonyesha kuwa na mafanikio na
wanafunzi wameupenda na wameweza kupata elimu bora.
Katika
kipindi cha miaka miwili ijayo mpango huu utatekelezwa katika makambi
mbalimbali ya wakimbizi nchini Kenya,Tanzania na Demokrasia ya watu wa Congo
lengo kubwa likiwa ni kuwafikia watoto 40,000 wanaoishi kwenye makambi ya
wakimbizi.
Akiongea
juu ya mradi huu Mkurugenzi wa taasisi ya Vodafone Foundation anasema: “Hadi
mwaka 2013,UNHCR ilitoa takwimu kuwa
inakadiriwa kuwa kuna wakimbizi kwenye kambi mbalimbali duniani wapatao milioni
50 na kati yao nusu yao ni watoto wenye umri chini ya miaka 18 na hali hiyo
inasababisha wapoteze ndoto ya kupata elimu.Mpango wa madarasa ya fasta wa
Vodafone ni tumaini jipya na utawezesha watoto wanaoishi kwenye mazingira
magumu kama haya kupata elimu”.
Naye
Afisa Mwandamizi wa UNHCR Olivier Delarue anasema:Kutokana na majanga yanayojitokeza na kusababisha kundi kubwa kuishi nje ya
utaratibu wa maisha yao ya kawaida,UNHCR inakabiliwa na changamoto mbalimbali
kuwapatia mahitaji mbalimbali ya kibinadamu ikiwemo elimu.Tunakaribisha ubunifu
huu wa taasisi ya Vodafone katika kutoa elimu kwa wakimbizi na tuko tayari
kufanya kazi na taasisi hii katika kukabiliana na changamoto nyingine
tunazokabiliana nazo.”
masanduku maalum yanayobeba vifaa vya kufundishia ,kuzalisha nishati ya umeme,kuchaji vifaa vya kufundishia na modemu maalumu za interneti ambazo hazihitaji kuunganishwa papo kwa papo .Vifaa vyote hivi vilivyoandaliwa kwa ajili ya mpango huu unaoendeshwa kwenye maeneo yenye mazingira magumu vikiunganishwa kwa muda mfupi vinawezesha walimu maalumu walioandaliwa kuvitumia kuweza kuwapatia elimu wanafunzi bila matatizo yoyote.
Hata watoto wetu vijijini hawapati hii fursa. Ndio maana wakimbizi hawarudi kwao kisha sisi tunawapa uraia kushindana na wale walionyimwa fursa nchini kwetu!!! Kweli hujafa hujaumbika!!!!
ReplyDelete