Sheikh Shariff Majini kutoka jijini Dar es salaam ambaye kwa sasa yupo ziarani katika baadhi ya mikoa Tanzania Bara, Jumapili tarehe 28-05-2017 atafanya kongamano kubwa kwa ajili ya akina Mama wa Jijini Arusha katika ukumbi wa CCM Mkoa kuanzia saa mbili asubuhi.
Matayarisho yote yamekwisha malizika na Sheikh ameshawasili Jijini Arusha tayari kabisa kwa ajili ya kuendesha kongamano hilo.

Pamoja na kongamano hilo Sheikh atafanya visomo kwa ajili ya kuwaombea watoto wanafunzi wa Shule ya Lucky Viscent ya Arusha waliofariki katika ajali ya gari. Pamoja na watoto watatu walionusurika wanaopata matibabu Marekani ili wapate nafuu haraka waweze kurejea kwenye masomo yao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...